Pichani ni Ndugu Pai Nyanzandoba akitoa mchango wake kuhusu utekelezaji wa PETS, katika moja ya warsha zilizofanyika Morogora katika ukumbi wa Flomi Hotel, warsha hiyo iliendeshwa kwa muda wa siku tatu na kuhudhuliwa na wanachama mbalimbali wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) kutoka mikoa sita.
MAANA YA PETS (public expenditure and tracking system)
PETS (Public Expenditure Tracking Survey) ni mfumo au utaratibu wa
wananchi kufuatilia fedha za umma
tangu zinapotolewa (Serikali kuu, n.k), kupitia halmashauri za
(wilaya/miji/manispaa/jiji) hadi ngazi ya matumizi ya mwisho. Kwa maelezo mafupi ni WANANCHI KUFUATA PESA zao zilizoelekezo katika matumizi ya bajeti.
SIFA ZA PETS
Ushirikishaji: pamoja
na Fuatilia pesa kuanzishwa na AZAKI, inatarajiwa kuwa mfumo huu utaendelezwa
kwa ushirikiano baina ya AZAKI, TAMISEMI na Mamlaka zote za Serikali za Mitaa
Kuanza Polepole na kwa Uangalifu: Kwa kuanzia PETS italenga kushughulikia
mtiririko wa raslimali na kujaribu kuonyesha jinsi fedha zinavyotumika. Hii itahusisha kushughulikia kwa ujumla kila chanzo
cha mapato, na matumizi katika halmashauri
Kurahisha Utoaji Taarifa: kufuatia kuwapo juhudi za
kutumia mfumo sanifu wa kompyuta wa PlanRep itakuwa rahisi kwa halmashauri
kutoa taarifa
Kusaidia na si kukagua: Kazi ya
PETS si kuwa aina nyingine ya ukaguzi wa mahesabu. Bali, inakusudia
kuufahamisha umma juu ya raslimali fedha zinazoletwa kwenye halmashauri, na
kuwasaidia kuelewa jinsi mchakato wa bajeti na matumizi vinavyosimamiwa
FAIDA
ZA PETS
• Itamuwezesha mwananchi kupata na kutumia
taarifa za fedha.
• Itamsadia mwananchi kuelewa uhusiano baina ya huduma zinazotolewa,
fedha zinazotengwa na matumizi halisi.
• Wananchi
wanaweza kutumia taarifa zitokanazo na PETS Kujua iwapo pakacha linavuja mahali
fulani katika mtiririko (wapi na kwa
kiasi gani). Mfano kulinganisha fedha iliyotolewa na serikali kuu, kiasi
kilichopelekwa wilayani, na kiasi kilichopelekwa ngazi ya kijiji. (mapungufu na
wapi yalipotokea )
• Kufahamu
chanzo cha matatizo : mf upungufu wa vifaa vya kufundishia: je serikali
haikutoa pesa? Je ugawaji ulikuwa mbovu?
• Kujua sababu za Serikali kuu au Halmashauri
kushindwa kutekeleza ahadi au mipango yake. Mfano Ahadi ya kujenga au kuboresha
darasa au maabara. Fedha kutokupatikana kabisa? Au kupatika kwa hela pungufu?
• Kuhakiki thamani halisi ya fedha. Mfano Je
Darasa iliyojengwa ina thamani ya Milioni 15?
TACEDE itakuwa bega kwa bega kuhamasisha jamii kutumia mfumo huu wa ufatiliaji fedha za umma.
No comments:
Post a Comment